Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KAMATI YA TAIFA STARS YATOA NAMBA YA SIMU KWA WADAU KUICHANGIA STARS.



 
Kamati ya Taifa Stars imeanza kufanya kazi yake baada ya hii leo kutoa rasmi namba ambayo itakuwa ikitumika katika masuala ya kuisaidia na kuichangia timu ya Taifa ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars.

Akiongea na waandishi wa habari, katibu wa kamati hiyoTeddy Mapunda amesema watanzania wanaweza kuichangia Taifa Stars kiasi chochote cha fedha kuanzia shilingi mia moja (TZS 100) kwenda namba 0654-888868 (Tigo Pesa) na 0789-530668 (Airtel Money) ambazo zitatumika kwa ajili ya motisha kwa wachezaji, uhamasishaji/masoko na maboresho ya kambi za ndani na nje ya nchi.

Aidha Teddy amesema Kamati ya Taifa Stars inaandaa utaratibu kwa ajili ya mashabiki watakaotaka kusafiri kuelekea nchini Algeria katika mchezo wa marudiano, waweze kuchangia gharama za usafiri ili waweze kwenda kuipa sapoti Stars katika mchezo wa marudaiano Novemba 1.

Kamati inawaomba watanzania, wadau, washabiki na wapenzi wa mpira miguu nchini kuichangia timu ya Taifa kupitia namba zilizotolewa na pia kujitokeza kwa wingi kuujaza uwanja wa Taifa siku ya mchezo wa tarehe 14 Novemba, 2015

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget