
Mchezo ulipangwa kucheza leo kati ya Mtibwa Sugar
dhidi ya Stand United umevunjika kutokana na mvua kubwa kunyesho huko Manugu
Mkoani Morogoro na hivyo kuendelea siku ya kesho.
Afisa habari wa Mtibwa Thobias Kifaru amesema mvua
hiyo ilikuwa kali hivyo kuahirishwa kwa mchezo huo lakini siku ya kesho
utaendelea kwa kipindi cha pili.
Kifaru amesema mchezo huo umevunjika hii leo lakini
klabu yake ilikuwa inaongoza kwa bao moja kwa bila hivyo wanaimani watafanya
vizuri zaidi siku ya kesho.
Post a Comment