Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

WENGER AMKOMALIA WILSHERE.



Image result for wilshere 
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema matumaini yake ni kwamba kiungo wa kati Jack Wilshere, ambaye kwa sasa ametumwa Bournemouth kwa mkopo, atasalia Arsenal maisha yake ya uchezaji.

Wilshere, mwenye miaka 24, ambaye huchezea timu ya taifa ya Uingereza, alienda Bournemouth kwa mkopo wa msimu mmoja.

Ni mmoja wa wachezaji waliokua kutoka chuo cha kustawisha wachezaji cha Arsenal na aliwachezea mechi yake ya kwanza 2008 akiwa na miaka 16.

Lakini alicheza mechi tatu pekee klabu hiyo msimu uliopita kutokana na majeraha na Wenger amesema walizungumza na mchezaji huyo kihusu mustakabari wake.

Bournemouth watakutana na West Bromwich Albion Jumamosi hii na Wilshere anatarajiwa kucheza.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget