Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

AZAM FC KUANZISHA MRADI MKUBWA WA SOKA LA VIJANA.



 

Timu ya Azam FC inatarajia kuanzisha mradi mkubwa wa kukuza soka la vijana unaojulikana kama ‘Azam FC Satelite Centre’ ili kuboresha soka la kitanzania.


Mradi huo utasimamiwa na Kocha Mkuu mpya wa Academy ya Azam FC, Tom Legg raia wa Uingereza, ambaye hivi karibuni alisaini mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi hicho.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba, amesema lengo kubwa la mradi huo ni kuzalisha wachezaji bora vijana watakaopata nafasi ya kuingia kwenye academy (Azam FC) na wengine kusajiliwa na timu nyingine.

Kawemba amesema kwa kuanzia tu mradi huo utaanza na vituo vitano vitakavyokuwa kwenye mikoa mitano tofauti nchini, kwenye kila mkoa zitaundwa timu nne za vijana za chini ya miaka 10,12,14 na16, huku akiongeza kuwa hadi kufikia mwaka 2025 wanataka wawe wamesambaza vituo hivyo nchi nzima.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget