Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

ROBBEN ATAKA MABADILIKO KATIKA TIMU YAKE YA TAIFA YA UHOLANZI.



 
Nahodha wa timu ya taifa ya Uholanzi, Arjen Robben amesema mchezo wao wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Wales ni nafasi ya kuanza kujijenga upya baada ya kushindwa kufuzu michuano ya Euro mwakani 2016.


Akihojiwa Robben amesema jambo pekee wanaloweza kufanya ni kujaribu na kuwanza kujijenga upya tayari kwa maandalizi ya mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018.



Uholanzi walishindwa kufuzu michuano hiyo kwa kumaliza katika nafasi ya nne katika kundi lao pamoja na kupangwa kama timu ya juu.

Robben mwenye umri wa miaka 31, toka wakati huo amechukua beji ya unahodha kutoka kwa Robin van Persie na anataka kuanza kwa kuifunga Wales ambao wamefuzu michuano hiyo.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget