Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

TWIGA STARS NGOMA INOGILEEEE.




 

Na Nicolaus Kilowoko.

Hatimaye Timu ya Taifa ya Tanzania kwa upande wa soka la wanawake, Twiga Stars imekata mzizi wa fitna baada ya hii leo kuitandika timu ya wanawake ya Malawi kwa mabao 2-0 katika dimba la Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam mchezo ambao ni wa kirafiki wa kimataifa.

Mchezo huu wa Twiga Stars ulikuwa ni sehemu moja wapo ya kumuaga mchezaji mwenzao ambaye aliyekuwa mwanzilishi wa timu hiyo kwa kipindi kirefu mkongwe, Esther Chaburuma ‘Lunyamila’.

Katika mchezo huu Twiga ilikuwa na moto wa aina yake kutokana na mchezo waliokuwa wanacheza kutokana na kasi ya mchezo huo na kuwamili wenzao wa Malawi.

Twiga Stars ilipata ushindi huo mnono wa mabao 2-0 kupitia kwa wachezaji wake mahiri na hatari kabisa Asha Rashid katika dk.43 lingine likiwekwa kimiani na Mwanahamisi Omar ‘Gaucho’ katika dk.82 ya mchezo.

Ikumbukwe tu katika mchezo huo kiingilio kilikuwa ni shilingi 1000 huku kikosi cha Twiga Stars kikiwa kinanolewa na kocha mzawa Rogasian Kaijage huku akiwataka watanzania wajitokeze kwa wingi katika kuisapoti timu hiyo kwa kuipatia udhamini wa kutosha.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget