Baada ya Mshambuliaji wa Tp Mazembe Mbwana Samatta
kupata timu nchini Ubelgiji sasa mchezaji wa klabu ya soka ya Azam FC Farid
Mussa nyota yake imeng’aa baaada ya kuhitajika nchini Slovakia.
Klabu ya Azam FC inaelekea Visiwani Zanzibar bila kuwa
na mchezaji huyo ambaye anaelekea nchini Slovakia kwaajili ya kufanya majaribio
ambayo kama akifanikiwa basi na yeye huenda akawa kati ya wachezaji mahiri
ambao wamepata bahati ya kucheza nje ya nchi.
Klabu ya Azam FCimekubali kumuachia mchezaji huyo
kwenda kwenye majaribio nje ya nchi hivyo kama mchezaji huyo atafuzu majaribio
hayo watahitaji kukaa mezani kujadiri hatma ya mchezaji huyo.
Baada ya Farid kuelekea majuu sasa nafasi yake
imechukuliwa na mchezaji Raadhani Singano ambae amekuwa akisugua benchi mara
nyingi tangu ahamie klabuni hapo akitokea katika klabu ya Simba.
Post a Comment