
Kikosi cha Yanga leo imefanya mazoezi yake katika
uwanja wa karume jijini Dara es Salaam kwaajili ya maandalizi yao kuelekea
katika michuano ya kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar
January mwakani.
Kocha Msaidizi wa klabu hiyo Juma Mwambusi amesema
maandalizi yanazidi kupamba moto kujiandaa na michuano hiyo huku akijitapa
kufanya vizuri katika michuano hiyo kutokana na kundi ambalo wamepanga katika
kombe hilo.
Mwambusi amesema kutokana na kiwango cha Yanhga
walichokionyesha katika mchezo wao uliopita dhidi ya Mbeya City na kuonyesha
kiwango kizuri cha kushinda mabao 4-o mchezo uliochezwa katika dimba la uwanja
wa Taifa jijini Dar es Salaam hivyo anakiamini kikosi chake.
Post a Comment