Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

CANNAVARO ATOA YAKE YA MOYONI BAADA YA SAMATTA KUTANGAZWA NOHODHA MPYA WA STARS.



Breaking News: Nadir Haroub astaafu kuchezea Stars 

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ na klabu ya soka ya  Yanga Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ameamua kustaafu kuichezea timu hiyo ili kuweka nguvu kwenye klabu yake Yanga.


Cannavaro ameiambia amesema kwa sasa ana mambo mengi yanayomfanya ajiondoe kuichezea timu hiyo moja wapo ni kitendo kilichofanywa na kocha mkuu wa timu hiyo Charles Boniface Mkwassa kumteua mshambuliaji Mbwana Samatta kuwa nahodha bila kumpa taarifa kabla.

Jambo jingine Cannavaro amesema ni lawama anazopata kutoka kwa mashabiki ambao wanadai yeye ndiye anayeifungisha timu hiyo pale inapopata matokeo mabovu.

Cannavaro anasema maneno yamekuwa mengi na yalianza mara baada ya mechi ya marudiano ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia dhidi ya Algeria kule kwao.

“Katika mechi hiyo tulifungwa mabao 7-0, mechi hiyo muda mwingi tulijitahidi kupambana kuhakikisha tunawatoa Algeria lakini ikashindikana, cha ajabu mara baada ya mechi hiyo nilionekana mimi pekee ndiye niliyefungisha,”Alisema Canaavaro.

Cannavaro kwa sasa ameamua kujiwka pembeni baada ya kocha mkuu wa Taifa Stars Charles Boniface Mkwasa kumtangaza Samanatta kama nahodha mpya.

Cannavaro amesema amepeleka barua rasmi kwa Shirikisho la soka nchini Tnzania TFF ya kuwapa taarifa ya kustaafu kwake kuichezea timu ya taifa.


Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget