
Mabingwa watetezi wa mashindano ya tenisi ya
Australian Open Novak Djokovic na Serena Williams wamefuzu kwa raundi ya tatu
ya mashindano hayo.
Pamoja na mabingwa hao kushinda lakini Nyota
mwingine Petra Kvitova hata hivyo ameshindwa kufuzu katika mashindano hayo.
Mchezaji nambari moja duniani upande wa wanawake
Williams alimtoa raia wa Taiwan Hsieh Su-Wei 6-1 6-2 naye Djokovic akamondoa
Mfaransa Quentin Halys kwa kumshinda 6-1 6-2 7-6 (7-3).

Roger Federer na Maria Sharapova pia wamesonga
kwenye mashindano hayo yanayoendelea Melbourne.
Lakini bingwa mara mbili wa Wimbledon Kvitova
wameshindwa 6-4 6-4 na raia wa Australia Daria Gavrilova mwenye umri wa miaka
21.
Nyota wa Uingereza Andy Murray na Johanna Konta
watarejea uwanjani raundi ya pili Alhamisi.
Post a Comment