
Baada ya kurejea kutoka Mafinga kwenye kombe la FA walipocheza
dhidi ya klabu ya Lipuli na kupata ushindi wa bao 1-0 sasa klabu ya soka ya JKT
Ruvu kesho inajitupa dimbani katika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam
katika mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya klabu ya Maji maji.
Akizungumzia hali ya kikosi chake kocha msaidi wa
klabu ya JKT Ruvu Mrange Kabange amesema wachezaji wake wote wana morali nzuri zaidi
katika mchezo huo baada ya kupata ushindi huo katika kombe la FA hivyo
mashabiki wake wakae mkao wa kula tu siku ya kesho.
Klabu ya JKT Ruvu inashuka dimbani huku ikiwa na
kumbukumbu ya kupoteza michezo miwili mfululizo ya liki kuu dhidi ya mnyama Simba
na maafande wenzao Mgambo Shooting katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaaam.
Wakati JKT Ruvu ikishuka dimbani siku ya kesho ikiwa
katika hali mbaya nayo klabu ya soka ya Maji maji inashuka katika uwanja wa
karume huku na wao wakiwa dhohofu ini hali baada ya kupata matokeo yasiyo
ridhisha katika mchezo wao wa mwisho wa Ligi kuu.
Post a Comment