
Mchezaji nyota wa mchezo wa tenisi kutoka nchini Uingereza Johanna Konta amemshinda nyota machachariwa mchezo huo Venus Williams kwa seti 6-4 6-2 na kufika raundi ya pili ya shindano la tenisi la Australian Open mjini Melbourne.
Konta, 24, alipata ushindi kwa kutumia dakika 79 huku bingwa wa Grand Slam Williams.
Baaada ya mchezo huo kumalizika na Konta kushina alisema baada ya kuona Droo ilipofanywa na akaona alikuwa amepangwa kucheza na Venus aliomba afanye vizuri bila kufungwa mapema.
Konta, aliyefika hatua ya 16 bora katika US Open mwaka 2015, sasa atakutana na mshindi kati ya Carina Witthoeft na Saisai Zheng, katika raundi ya pili.

Konta aliyeorodheshwa nambari 47 duniani, alikuwa akicheza mara ya kwanza katika Australian Open na ndiye mwanamke Mwingereza pekee aliyesalia katika droo ya mashindano ya mchezaji mmoja mmoja baada ya Heather Watson kushindwa Jumatatu iliyopita.
Kwa upande wa wanaume mchezaji Andy Murray pia alishinda lakini Dan Evans akabanduliwa huku mchezaji mwingine Aljaz Bedene akisubiriwa kucheza muda mfupi kuanzia sasa atacheza baadaye.
Post a Comment