Klabu ya soka ya Mtibwa Sugar ya Manungu turiani Mkoani
Morogoro imejinasibu kufanya vizuri na kutuma salamu kwa klabu ya soka ya Simba
katika mchezo wao wa kesho utakaopigwa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaaam.
Kocha mkuu wa klabu hiyo Mecky Mexime amesema amejipanga
vyema katika mchezo wao wa kesho dhidi ya wapinzani wao hao huku akijisifu
kuwasoma vizuri Simba walipokutana katika Kombe la mapinduzi Visiwani Zanzibar.
Mchezo wa kesho unatarajiwa kuwa mgumu kutokana na klabu
zote mbili zinakutana kwa mara ya pili katika Ligi kuu soka Tanzania bara baada
ya kukutana katika kombe la mapinduzi huku klabu ya Simba ikitolewa na Mtibwa katika
hatua ya nusu fainali.
Mtibwa yenyewe ilitolewa katika hatua ya fainali
baada ya kufungwa mabao 3-1 na watoza ushuru wa URA ya Uganda.
Mexime amesema pamoja na kutolewa na timu ya URA ya
kutoka nchini Uganda lakini kwa sasa hawageuki nyuma kuangalia makosa
yaliyofanyika ila wanachoangalia kwa sasa ni mchezo wao wa kesho ambao umeteka
hisia kuwa ya mashabikia wa soka nchini.
Post a Comment