
Mino Raiola ambaye ni wakala wa
kiungo wa klabu ya Juventus Paul Pogba amekanusha tetesi kuwa Barcelona ndio
wenye nafasi ya kumsajili kiungo wa huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwishoni mwa
msimu huu.
Raiola amesema Pogba amekuwa mmoja
kati ya wachezaji wanaowindwa zaidi duniani toka alivyojiunga na Juventus kwa
uhamisho huru akitokea Manchester United majira ya kiangazi mwaka 2012.
Nyota huyo amefanikiwa kushinda
mataji matatu ya Serie A akiwa na Juventus na kutinga hatua ya fainali ya
michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita.
Na klabu ya Juventus bado ina
mkataba na Pogba unaomalizika mwaka 2019 lakini ofa kutoka katika klabu kubwa
zinaweza kutolewa katika kipindi cha kiangazi.
Post a Comment