Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

CARRAGHER:ARSENAL WASIPOTWAA TAJI MSIMU HUU BASI PASI ZA OZIL HAZINA MAANA.



 

Gwiji wa zamani wa klabu ya soka ya Liverpool Jamie Carragher ameanza kuichambua Arsenal na kusema kuwa pasi nyingi za mabao za kiungo Mesut Ozil zitakuwa si kitu iwapo Arsenal itashindwa kunyanyua taji la Ligi ya Uingereza mwezi Mei mwaka huu.


Mjerumani huyo ametajwa kuwa mchezaji wa Arsenal aliyefanya kazi kubwa msimu huu, baada ya kufikisha pasi 16 zilizozaa magoli, ni tishio sasa kwani anakaribia kuvunja rekodi ya Thierry Henry ya pasi 20. 

Hata hivyo, nahodha wa zamani wa Liverpool, Carragher amesisitiza kuwa vijana hao wa Arsene Wenger wanahitaji kushinda taji kubwa la Uingereza ili kuifanya kazi nzuri ya Ozil ionekane kuwa na tija.

“Hesabu zake zinaonekana Anaelekea kuvunja rekodi lakini kama hatapata medali, itakuwa na maana gani?",alisema Carragher.

Washika Mtutu wamejitwalia Kombe la FA mfululizo tangu ujio wa Ozil mnamo 2013, Lakini Arsena ina changamoto kubwa ya kuusaka ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza ambao waliutwaa kwa mara ya mwisho 2004.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget