
Klabu ya soka ya Mashetani wekundu ya Manchester
United inaripotiwa kuingia katika mbio za kumuwania mshambuliaji wa Sporting
Lisbon Islam Slimani baada ya nyota huyo anayekadiriwa kuwa na thamani ya
paundi milioni 13 kufunga mabao 13 katika mechi 16 msimu huu,imelipoti The Sun.
Kocha Mkuu wa Real Madrid, Zinedine Zidane amemuwek kiungo wa Juventus Paul Pogba katika orodha yake ya juu katika usajili wa majira yajayo ya kiangazi,imelipoti Tuttosport.
Galatasaray imeungana na Inter Milan, Chelsea na
barcelona katika mbio za kumuwania Ezequiel Lavezzi ambaye amepanga kuondoka
Paris Saint-Germain pindi mkatab wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu
huu,imelipoti Calciomercato.com
Atletico Madrid inatajwa kukaribia kumuongeza mkataba Antonie Griezmann ambao utafanya mshahara wake kuongezeka na ada ya kuvunja mkataba kupaa kutoka euro milioni 80 mpaka 100. Klabu za Paris saint-Germain na Real Madrid zote zinatajwa kumuwania,imelipoti AS
Atletico Madrid inatajwa kukaribia kumuongeza mkataba Antonie Griezmann ambao utafanya mshahara wake kuongezeka na ada ya kuvunja mkataba kupaa kutoka euro milioni 80 mpaka 100. Klabu za Paris saint-Germain na Real Madrid zote zinatajwa kumuwania,imelipoti AS
Post a Comment