
Imeripotiwa kuwa hali ya afya ya Nguli wa zamani wa
soka wa Brazil, pele inaendelea vyema kufuatia upasuaji mdogo wa nyonga
aliofanyiwa kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa jana.
Pele mwenye umri wa miaka 75 na mshindi mara tatu wa
Kombe la Dunia alifanyiwa upasuaji huo Desemba 3 mwaka jana jijini New York.
Afisa habari wake, Pepito
amesema Pele alitumia muda wake wa mapumziko aliokuwa na mabinti zake na
wajukuu zake huko New York na kufanyiwa upasuaji huo.
Mwaka 2012 Pele alifanyiwa upasuaji mwingine kama
huo huku mwaka jana akitumia zaidi ya wiki mbili hospitali baada ya kufanyiwa
upasuaji wa kidole tumbo.
Post a Comment