
Klabu za Real Madrid na Atletico Madrid zimeonyeshwa
kuchukizwa kufungiwa mwaka mmoja kusajili wachezaji wapya na Shirikisho la Soka
Duniani-FIFA jana, na kutangaza nia yao ya kukata rufani.
Klabu zote mbili zimelimwa adhabu hiyo kufuatia
kukiuka sheria ya usajili wa wachezaji wa kigeni wenye umri wa chini ya umri wa
miaka 18.
Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wake,
Madrid wamedai kuwa watapinga umuzi huo wa FIFA katika mamlaka zote za soka.
Naye rais wa Atletico Enrique Cerezo amesema pamoja
na kuwa wanaweza kukabiliana na adhabu hiyo kutokana na kikosi walichonacho
lakini watakata rufani kwasababu wanaamini hawakutendewa haki katika maamuzi
hayo.
Real na Atletcio pia wamepigwa faini ya dola 358,000
na 895,000 na kupewa siku tisini kurekebisha suala hilo.
Post a Comment