Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

LIGI DARAJA LA KWANZA KUENDELEA TENA SIKU YA KESHO.



 
Ligi Daraja la Kwanza kwa siku ya kesho kwa michezo 12 kuchezwa katika viwanja mbalimbali, huku timu 3 za juu kutoka katika kila kundi zikipata nafasi ya kupanda Ligi Kuu msimu ujao moja moja.


Kundi A, Jumamosi Mji Mkuu watawakabili Africa Lyon uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, KMC dhidi ya Kiluvya uwanja wa Mabatini Mlandizi, Polisi Dodoma watacheza dhidi ya Friends Rangers uwanja wa  Mgambo Mpwapwa, huku Jumapili Polisi Dar wakiwakaribisha Ashanti uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Kundi B, Njombe Mji watakua wenyeji wa Kimondo uwanja wa Amani Njombe, Lipuli FC dhidi ya Kurugenzi uwanja wa Wambi – Mafinga,
Uwanja wa Majimaji mjini Songea JKT Mlale watakua wenyeji wa Polisi Morogoro, huku Jumapili kukichezwa mchezo mmoja Ruvu Shooting dhidi ya Burkinafaso uwanja wa Mabatini, Mlandizi.

Kundi C, Rhino Rangers watawakaribisha JKT Kanembwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Panone FC dhidi ya Geita Gold uwanja wa Ushirika mjini Moshi, uwanja wa Karume Musoma, wenyeji Polisi Mara watacheza dhidi ya Polisi Tabora, huku siku ya Jumapili Mbao FC wakiwakaribisha JKT Oljoro uwanja wa CCM Kirumba.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget