Ligi kuu soka Tanzania bara inatarajiwa kuendelea
tena siku ya kesho katika viwanja kadha wa kadha nchini huku klabu ya soka ya
Mgambo JKT ikijitamba kwapigisha kwata maafande wenzao klabu ya JKT Ruvu.
Kocha mkuu wa klanu ya soka ya Mgambo Bakari Shime
amesema ligi kwa sasa imebadirika kutokana na kila timu kujipanga kufanya
vizuri katika ligi hiyo hali ambayo inaongeza ushindani ndani ya ligi hiyo.
Shime amesema pamoja na kuanza vibaya katika ligi hiyo msimu huu lakina anaimani na kikosi chake kutokana na jinsi ambavyo anavyokiongoza na jinsi wanavyofata maelekezo yake huku akiitaka klabu ya JKT Ruvu kukaa sawa katika mchezo wao wa kesho.
Post a Comment