
Kocha wa Manchester United, Louis
van Gaal amesema hakuna miujiza ya kuimarisha hali ya klabu hiyo zaidi ya timu
nzima kwa ujumla kujituma na kuongeza bidii.
Akihojiwa Van Gaal amesema jambo
muhimu wanaloweza kufanya ni kuangalia walipokosea na kuona jinsi gani wanaweza
kuboresha kama timu ili waweze kupata matokeo wanayohitaji.
United wamecheza mechi nane bila
kushinda hata moja, sita zikiwa Ligi Kuu hivyo kuwafanya kuporomoka mpaka
nafasi ya sita katika msimamo.
Lakini Mbali na kushuka katika
msimamo pia wameng’olewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na kuangukia
katika michuano ya Europa League.
Post a Comment