
Mlinda mlango wa Arsenal, Petr Cech
amekiri kupania kuendeleza rekodi yake ya kutofungwa na nyota wa Barcelona
Lionel Messi.
Akihojiwa Cech amesema ni jambo
kubwa kwa kuwa sio makipa wengi ambao wamewahi kucheza na Messi katika mechi
nane na hajawafunga.
Wawili hao wamekutana mara kadhaa
wakati Cech akiwa Chelsea ambapo katika mechi nane walizokutana Messi
hajafanikiwa hata mara moja kumfunga golikipa huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya
Czech.
Nyota hao wanatarajiwa kukutana tena
wakati Arsenal watakapovaana na Barcelona katika hatua ya timu 16 bora za michuano
ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwezi ujao.
Post a Comment