Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

YANGA KESHO DIMBANI TENA,TAIFA.



 

Klabu ya soka ya Young Africans siku ya kesho watawakaribisha timu ya Friends Rangers katika dimba la uwanja wa Taifajijini Dar es Salaam.

Yanga inashuka dimbani kesho ukiwa ni Mchezo huo ni wa kombe la shirikisho baaada ya kusimam kwa ligi kuu soka Tanzania bara.

Michezo mingine ya kombe hilo ni Njombe Mji watakua wenyeji wa Tanzania Prisons katika uwanja wa Amani Njombe, huku Stand United wakicheza dhidi ya Mwadui FC katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Michuano hiyo itaendelea Jumatatu, Kagera Sugar wakiwa wenyeji wa Rhino Rangers katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora, Panone FC dhidi ya Madini FC uwanja wa Ushirika mjini Moshi na Africa Lyon wakiwa wenyeji wa Azam FC uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Jumanne Mtibwa Sugar watawakaribisha Abajalo FC uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, Lipuli dhidi ya JKT Ruvu uwanja wa Wambi Mafinga, Africa Sports dhidi ya Coastal Union Mkwakwani jijini Tanga, na Geita Gold watakua wenyeji wa Mgambo Shooting katika uwanja wa Nyankumbu mjini Geita.

Singida United watacheza dhidi ya Mvuvuma siku ya Jumatano katika uwanja wa Namfua mjini Singida, na mchezo wa mwisho utachezwa Februari Mosi katika ya Wenda FC dhidi ya Mbeya City uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget