Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

VIERA AMPONDA MZEE WENGER HUKU AKIMPA TANO MOURINHO.



Vieira: Mourinho impressed me more as a manager than Wenger 

Kuelekea katika kipute cha kesho kinachozikutanisha klabu hasimu zaidi nchini Uingereza klabu ya Arsenal dhidi ya Chelsea mchezaji wa zamani wa klabu ya soka ya Arsenal Patrick Vieira amemponda bosi wake wa zamani Arsene Wengwer.


Viera amesema aliyekuwa kocha wa zamani wa klabu ya soka ya  Chelsea Jose Mourinho ni bora zaidi kuliko kocha wake wa zamani  babu  Arsene Wenger.

Mchezaji huyo ambaye ameitumikia The Gunners kwa miaka 9 ameshinda makombe matatu ya Ligi na makombe manne ya FA Cup kabla ya kutimkia katika klabu ya Juventus na baadae Inter ambapo alifanya kazi kwa muda na Mourinho.

Viera ambaye ni raia wa nchini Ufaransa amesema amefanya kazi na Mourinho kwa muda lakini ameona ni bora zaidi kuliko kocha wake huyo wa zamani wa Arsenal.

Akihojiwa Viera amesema Mourinho ndiye aliyemfanya apende kazi yake ya ukocha na alikuwa alikuwa anajua mazuri na mabaya ya soka.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget