
Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Manchester City,
Kun Aguero ameteuliwa kuwa mwanasoka bora wa Ligi Kuu England kwa mwezi Januari.
Aguero raia wa Argentina amebeba tuzo hiyo baada ya
kufungia mabao matano klabu yake katika mechi nne za mwezi huo.
Aguero alikuwa majeruhi kabla ya kurudi tena dimbani
kusakata kabumbu na alikuwa akihusisha na kuihama klabu yake na kuelekea nchini
Hispani katika klabu ya Real Madrid.
Naye Ronald Koeman ameshinda tuzo ya kocha Bora wa
Mwezi Januari England, baada ya kuiongoza Southampton kuzifunga Watford, West
Brom na Manchester United.
Post a Comment