
Mashabiki wa klabu ya soka ya Simba wametoa maoni
yao mbalimbali kuhusu mwenendo wa klabu yao kwa hivi sasa baada ya klabu hiyo
kuonyesha makali katika ligi kuu soka Tanzania bara kwa michezo mitano
mfululizo.
Wadau hao wamesema mwenendo wa klabu yao hivi sasa
unaridhisha baada ya uongozi wa klabu hiyo kumtimua aliyekuwa kocha mkuu wa
klabu hiyo Dlyan Kerr na kumuachia kocha msaidizi Jakson Mayanja.
Klabu ya soka ya Simaba February 7 mwaka huu
inashuka dimbani kukipiga na klabu ya soka ya Kagera Suger katika mchezo wa
Ligi kuu soka Tanzania bara.
Post a Comment