Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SDL KUNA KAZI YAKE ILI KUINGIA FDL.

 
Raundi ya saba ya Ligi Daraja la Pili nchini (SDL) inaendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa nchini, kwa timu 24 kusaka pointi kutoka makundi ya A,B,C na D kuwania nafasi nne za juu ili kuweza kupanda ligi daraja la kwanza msimu ujao.


Kundi B, Kesho Jumamosi AFC ya Arusha watakua wenyeji wa Alliance Schools uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Madini FC watacheza dhidi ya JKT Rwamkoma uwanja wa Mbulu, huku Bulyanhulu FC watawakaribsiha Pamba FC uwanja wa Kamabrage mjini Shinyanga.

Kundi C, Leo Ijumaa Abajalo Dar watacheza dhidi ya Mshikamano uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, kesho Jumamosi Kariakoo FC watawakaribisha Changanyikeni katika uwanja wa Ilulu – Lindi, na Cosmopolitani watacheza dhidi ya Villa Squad siku ya jumatatu katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Kundi D, Jumamosi Mighty Elephant watacheza dhidi ya Wenda FC uwanja wa Majimaji mjini Songea, Mbeya Warriors watawakaribisha Mkamba Rangers uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, huku Jumapili Sabasaba FC wakicheza dhidi ya African Wanderers uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget