Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

CHINA KUNANI TENA,MAANA MARTINEZ NAYE HUYOOO...



 
Klabu ya soka cha Uchina ,Guangzhou Evergrande, kimevunja rekodi ya nchi hiyo kwa kima cha fidia ya kumsajili mchezaji katika timu yao.


Klabu hiyo imelipa dolla million 45 kusajili huduma za mshambuliaji wa kutoka Colombia,Jackson Martinez.

Martinez ambae sasa ameihama timu ya uhispania Atletico Madrid ametia sahihi kandarasi ya miaka minne.

Aliwahi kuifungia Atletico mabao 22 baada ya kuhamia Uhispania kutoka Porto na yeye ndiye mchezaji wa kiwango chake kuhamia Uchina baada ya kiungo cha kati wa Chelsea Ramires kuhamia Jiangsu Suning.

Kwa kutumia kitita kikubwa namna hiyo sasa ligi kuu ya Uchina inaikurubia ligi ya Uingereza kwa kima cha fedha zinazotumuka katika kuendesha soka nchini humo.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget