
TIMU ya Mali imekata tikiti ya kushiriki fainali ya
mchuano wa kuwania ubingwa wa Afrika CHAN baada ya kuilaza Ivory Coast 1-0
katika nusu fainali ya pili iliyochezwa katika uwanja wa taifa wa Rwanda.
Mali ambayo ilikuwa imefuzu kwa nusu fainali yake ya
kwanza ya CHAN ilipata bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika mbili tu mechi
hiyo imalizike.
Bao hilo lilitiwa kimiani na yves bissouma kunako dakika ya 88'ya
kipindi cha pili cha mchezo.
Bissouma alipata bao hilo kupitia pasi safi kutoka
kwa Sinayoko naye hakusita alipiga chenga moja na kumbwaga kipa wa The
Elephants Badra .
.
Post a Comment