
KOCHA mkuu wa klabu ya soka ya Arsenal Arsene Wenger
ameanza kuangalia mbadala wa Nahodha mpya ndani ya kikosi chake baada ya Nahodha wake wa sasa Mikel Arteta kuwa na uwezekano wa kutimka klabuni hapo mwishoni mwa
msimu huu.
Mzee Wenger ameanza kumuangalia mlinda mlango wake Petr
Cech kuwa Nahodha mpya ndani ya klabu ya soka ya Arsenal.
Wakati kiungo wa Arsenal Mikel Arteta akionekana kutaka
kuondoka Emirates Stadium mwezi June mwaka huu , Mzee Arsene Wenger anaangalie
mtu wa kuchukua nafasi yake klabu hapo.
Paoja na hayo lakini mlinda mlango namba moja nadani
ya klabu hiyo Cech, anaonekana ana nafasi
kubwa ya kuchukua nafasi hiyo kutokana na kuonekana kuweza kuimudu nafasi hiyo.
Cech's anaonekana anafasi hiyo kubwa kutokana na
kuwa na uwezo wa kuzungumza Lugha 5 kwa wakati mmoja na kuwa na maamuzi mzuri
katika kikosi hicho tangu ajiunge nacho akitokea Chelsea.
Post a Comment