Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

YANGA KUJITUPA UWANJANI SIKU YA KESHO KUWAVAA WA RWANDA.



 
Kikosi cha Yanga jumamosi hii kinatarajiwa kushuka dimbani katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuvaana na timu ya APR ya kutoka nchini Rwanda.

Yanga inashuka dimbani kucheza na APR katika dimba la uwanja wa Taifa ka ajili ya kutafuta tiketi ya kushiriki Fainali za kombe la klabu bingwa Afrika.

Katika mchezo wao wa kwanza uliopigwa katika dimba la Amahoro Kigali nchini Rwanda Yanga ilipata ushindi wa mabao 2-1 na kuifanya kuongeza matumaini ya kupata ushindi zaidi jumamosi hii na kuifanya isonge mbele.

Wakati Yanga wakijitupa jumamosii hii dimbani, siku Jumapili Azam FC watakua wakicheza dhidi ya Bidvest FC kutoka nchini Afrika Kusini katika mchezo wa Kombe la Shirikisho (CAF CC) kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi. 

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limezitakia kila la kheri vilabu wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa, timu za Azam FC na Yanga SC katika michezo yao watakayocheza wikiendi hii.

Katika salamu hizo, TFF imezitakia kila la kheri timu hizo kuhakikisha zinafanya vizuri katika michezo yao ili ziweze kusonga mbele katika hatua inayofuata, na kuwapa furaha washabiki wa mpira wa miguu pamoja na watanzania wote.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget