Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

TWIGA STARS KUKWEA PIPA LEO HII KUWAFATA WAZIMBABWE KATIKA MCHEZO WAO WA MARCH 20.



 
                               picha kwa msaada wa TFF.

Timu ya soka ya wanawake Twiga Stars imeeondoka ijumaa hii kuelekea nchini Zimbabwe kuwafata wazimbabwe katika mchezo wa marudiano wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afrika kwa upande wa wanawake.

Kocha mkuu wa Timu ya Twiga Stars Nasra Juma amesema kuelekea katika mchezo wao huu kikosi chake kimejiaandaa vyema na wanaimanai watashinda na kusonga mbele akatika hatua inayofata ya kushiriki michuano hiyo kwa upande wa wanawake.

Tigwa Stars inasafiri kuelekea nchini Zimbabwe kucheza mchezo wake huo huku ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wake kwanza katika dimba la uwanja wa Azam Complex uliopo chamazi jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo wa Twiga Stars na timu ya Zimbabwe unatarajiwa kupigwa march 20 mwaka huu nchini Zimbabwe.

Mkuu wa msafara ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Wanawake TFF, Amina Karuma, benchi la ufundi litaongozwa na kocha mkuu Nasra Juma, kocha msaidizie Elyutery Muholery, kocha msaidizi Edina Lema, daktari wa timu Anange Lwila, mtunza vifaa Esther Chaburuma na meneja wa timu Furaha Francis.

Wakati timu ya Twiga ikisafiri ijumaa hii nao kaka zao Taifa Stars inatarajiwa kuondoka siku ya jumamosi kuelekea nchini Chad kwaajili ya kuwafata wa Chad katika mchezo wao wa kuwania kufuzu fainali za Afrika kwa upande wa wanaume.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget