Timu ya Taifa ya soka la ufukweni ( BEACH SOCCER) inatarajiwa kuingia kambini Jumatano hii kwaajili ya kujiandaa na mchezo wake dhidi ya timu ya Taifa ya Ivory Cost mchezo utakaopigwa katika dimba la maalumu lililotengenezwa maeneo ya karume jijini Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa timu hiyo John Mwansasu amesema kuwa mpaka kufikia hii leo vijana wake wanaendelea vyema na kamabi hiyo itaanza rasmi Jumatano hii baada ya kuwajumuisha wachezaji kutoka visiwani Zanzibar.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Ijumaa hii huku wito ukitolewa kwa watanzania kuisapoti timu hiyo katika mchezo wao huo.
Post a Comment