Timu ya Taifa ya soka la vijana umri chini ya Miaka 17 SERENGETI BOYS baada ya kuwatandika Afrika Kusini mabao 2-0 sasa yaelekea nchini Madagasca kwaajili ya kuweka kambi tayari kujiandaa na mchezo wao unaofata dhidi ya Congo Brazaville.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Afisa habari wa Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF Alfred Lucas amesema kuelekea huku kuweka kambi ni moja ya ahadi waliyopewa na Rais wa TFF Jamal Malinzi endapo ingefanikiwa kuitoa Afrika Kusini.
Lucas amsema timu hiyo imeondoka bila kocha wake Mkuu Bakari shime ambaye amebaki kwa ajili ya kuendelea na kupata kozi ya Leseni B kwa ajili ya kujiweka vizuri zaidi kielimu.
Post a Comment