
KOCHA mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Charles Biniface Mkwasa kesho anatarajiwa kutangaza kikosi kwaajili ya mchezo wao wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika dhidi ya Nigeria.
Mkwasa anatarajiwa kutangaza kikosi cha wachezaji 20 huku pia kikisheeni zaidi vijana ambao wanatarajiwa kupatiwa uzoefu zaidi wa michuanao ya kimataifa.
Mbali na kucheza mchezo huo kwa upande wa Tanzania hatuna cha kupoteza sani kutokana na kuwa ni wazi tayari wenzetu Misri wameshafanikiwa kufuzu hatua hiyo hivyo tunaenda kucheza tukikwepa adhabu pamoja na kuipa timu yetu uzoefu zaidi.
Post a Comment