Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KAIKE ASEMA MAPAMBANO ALIYOYAANDAA YAPO PALE PALE DISEMBA 25 MWAKA HUU.



Image result for kaike silaju 
Pambano la masumbwi lisilo na ubingwa kati ya bondia Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’ na Francis Cheka lililopangwa kufanyika Desemba 25, mwaka huu litakuwepo kama lilivyopangwa.

Pambano hilo ambalo litapigwa kwenye ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es salaam, lilikuwa kwenye sintofahamu baada ya kukumbwa na mgogoro kwa upande wa waandaaji.

Promota wa mapambano hayo Kaike Silaju amesema kuwa maandalizi yote kuelekea katika pambano hilo yamekamilika na wapenzi wa mchezo huo wasubiri burudani tuu kutokana na mabondia wote kujiaandaa vyema.

Naye mmoja wa mabondi wa pambano hilo Twaha Kiduku amesema kwa upande wake amejipanga vyema sana kuelekea katika pambano hilo na anaimani anaweza kumshinda mpinzania wake.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget