Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KOCHA KIBADENI ATAKA MABADILIKO NDANI YA KIKOSI CHA JKT RUVU.



 
Kocha Mkuu wa klabu ya soka ya  JKT Ruvu Abdallah Kibadeni amekiri na kuwa safu yake ya ushambuliaji kikosini hao kuwa nib utu na inatakiwa ifanyiwa marekebisho ya haraka zaidi.

Kibadeni ameyasema hayo baada ya kutoka nayo sare ya bila kufungana na klabu ya soka ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara uliopigwa katika dimba la uwanja wa karume jijini Dar es Salaam juzi.

Amesema kikosi cha hivi sasa kinawachezaji wengi wapatao 30 na kinaitaji marekebisho makubwa ya kufumua kikosi cha kwanza ili kupata kikosi ambacho kitakuwa imara zaidi katika ushindani wa ligi kuu.

Kibadeni amechukua nafasi ya Fred Minziro aliyejiuzulu kutokana na matokeo mabovu ya timu hiyo.

Lakini paoja na matokeo hayo klabu ya JKT Ruvu ipo mkiani mwa ligi kuu ikiwa na pointi mbili tu katika mechi saba ilizocheza hadi sasa.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget