Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MKWASA ATANGAZA KIKOSI CHA WACHEZAJI 28 WA STARS WATAKAOWAVAA ALGERIA NOVEMBA 17.

 
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wachezaji 28 wa timu ya taifa kilicho tayari kupambana na Algeria.

Stars itaivaa Algeria katika mechi mbili mfululizo kuwania kucheza Kombe la Dunia 2018, ikianza kwa kupambana nayo Novemba 17 jijini Dar es Salaam kabla ya kurudiana Novemba 17, ugenini.

Mkwasa amewaongeza kikosini washambuliaji Malimi Busungu wa Yanga SC na Elias Maguri katika kikosi kitakachomenyana na Algeria katikati ya mwezi ujao.

Mkwasa ametaja wachezaji 28 ambao wataoingia kambini kwa siku 10 nchini Oman kuanzia Novemba 1, mwaka huu kujiandaa na Algeria katika hotel ya Urban Rose.

Taifa Stars itamenyana na Algeria katika hatua ya mwisho ya mchujo wa kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Kombe la Dunia 2018 Urusi, baada ya kuitoa Malawi katika hatua ya kwanza.


Wachezaji hao kuwa ni makipa; Aishi Manula (Azam FC), Ally Mustafa ‘Barthez’ (Yanga SC) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar). 

Mabeki ni: Shomary Kapombe (Azam FC), Juma Abdul, Mwinyi Hajji Mngwali, Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondan (Yanga SC), Hassan Kessy, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Hassan Isihaka (Simba SC) na Salim Mbonde (Mtibwa Sugar).

Viungo ni; Himid Mao, Mudathir Yahya, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Frank Domayo (Azam FC), Jonas Mkude, Said Ndemla (Simba SC) na Salum Telela (Yanga SC).

Washambuliaji ni Mbwana: Samatta, Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Free State Stars, A. Kusini), Farid Mussa, John Bocco (Azam FC), Simon Msuva, Malimi Busungu (Yanga SC), Elias Maguri (Ruvu Shooting) na Ibrahim Hajib (Simba SC).

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget