Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

STARS KUONDOKA KESHO TAYARI KUWAKABILI THE FLAMES KATIKA MECHI YA MARUDIANO HUKO MALAWI.



 
Baada ya kuanza vizuri kwa timu ya Taifa Tanzania Taifa Stars kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya Malawi (The Flames) katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaaaam siku ya jana kikosi hicho kinatarajia kuondoka kesho nchini kuelekea Lilongwe Malawi.

Stars inaelekea nchini Malawi kucheza na timu hiyo ukiwa ni mchezo wao wa marudiano wa kusaka tiketi ya kufuzu fainali za Dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Uswiz mchezo utakopigwa Oktoba 9 mwaka huu.

Afisa habari wa TFF BARAKA KIZUGUTO amesema timu hiyo inaelekea nchini Malawi siku ya kesho ikiwa na wachezaji wake 24 pamoja na benchi la ufundi likiongozwa na kocha Mkuu CHARLES BONIFACE MKWASA.

Naye Rais wa TFF JAMALI MALINZI amekipongeza kikosi cha Stars kwa ushindi huo na kuwataka watanzania kuendelea kuwasapoti katika mchezo wao huo wa marudianio nchini Malawi.










Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget