Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

TASWA KUKABIDHI TUZO YA HESHIMA KWA RAIS KIKWETE.



 
Chama cha waandishi wa habari za michezo Tanzania TASWA, kinatarajia kufanya sherehe za kumuaga na kumpa tuzo ya heshima Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mh. Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete sherehe zitakazo fanyika oktoba 12 mwka huu.

Mwenyekiti wa TASWA JUMA PINTO amesema tuzo hizo ambazo hufanyika kila mwaka kwa mwaka huu zitakuwa tofauti kidogo kwani zitatumika kumuaga Rais Jakaya Kikwete na kumpa tuzo ya heshima kwa kuthamini mchango wake katika kipindi cha miaka 10 aliyokuwa madarakani.

Awali tuzo hizo zilikuwa zifanyike Oktoba 8 ila kwa sasa zitafanyika Oktoba 12, pamoja na tuzo hiyo ya heshima lakini kuna tuzo 10 za wachezaji bora waliofanya vizuri katika kipindi cha miaka 10, tuzo 5 kwa viongozi wa michezo na taasisi iliyochangia kukuza michezo katika kipindi cha miaka 10.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget