Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

BAADA YA KOCHA MATOLA KUBWAGA MANYANGA KLABU YA SOKA YA SIMBA WAJIANADAA KUITISHA KIKAO CHA KAMATI.



 

Baada ya Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola kuamua kubwaga manyanga ya kuachana na kazi yake ya kuinoa klabu ya soka ya simba uongozi wa klabu hiyo umesema utaketi muda wowote kujadili hatima ya taarifa za kocha huyo.


Akizungumzia sakataa hilo Afisa habari wa klabu ya soka ya simba HAJI MANARA amesema ni kweli kunataarifa za kocha huyo kubwaga manya lakini wao kama klabu wataketi kujadili taarifa ambayo kocha huyo ameiwasilisha kwa Rais wa klabu hiyo EVANS AVEVA.

Matola ambaye ni nahodha wa zamani wa klabu ya soka ya Simba, alifanya kikao cha na Rais wa klabu hiyo Evans Aveva lakini akashikilia msimamo wake wa kutaka kuachia ngazi.

MANARA amesema kilichopelekea Matola kuachia nagzai ni kutoelewana na Kocha mkuu wa klabu hiyo Dylan Kerr katika masuala mengi, jambo ambalo Matola halikumpendeza.


Kwa upande mwingine MANARA ameelezea kuogeza mchezaji mwingine katika kikosi chao huku ameitakia kila la kheri timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars katika mchezo wao wa jumamosi na kuwataka watanzia kujitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo huo.
 

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget