Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

FIFA YAMUONDOA MUSA BILITY KATIKA KINYANG'ANYIRO CHA URAIS.



 
Kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la soka duniani FIFA limemuondoa katika kinyang’anyiro cha Urais wa FIFA Musa Bility ambaye ni Rais wa chama cha soka cha nchini Liberia.


Bility amekuwa mmoja kati ya watu ambao wameomba kugombea nafasi ya Urais wa FIFA kuchukua nafasi ya aliyekuwa Rais wa Shirikisho hilo Sepp Blatter ambaye ameamua kujiuzulu hivi karibuni.

Kamati ya uchaguzi imeamua kumuondoa Musa Bility kwa sababu za Uadilifu baada ya kumchunguza na kujiridhisha kuwa Bility hana sifa ya kubaki kuwa mgombea wa Urais katika uchaguzi mkuu wa FIFA mwezi wa pili tarehe 26 mwaka huu.

Mwingine aliyeondolewa katika kinyang’anyiro hicho ni Rais wa UEFA Michel Platini.

Michel Platini ameondolewa katika kuwania nafasi ya Urais kwa sababu amefungiwa na kamati ya maadili ya FIFA kwa muda wa siku 90 kwa kosa la kuhusika kupokea rushwa toka kwa aliyekuwa Rais wa FIFA Sepp Blatter.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget