Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SIMBA YAWACHIA WACHEZAJI WAKE HAO RASMI.



 

Klabu ya soka ya Simba hatimae hii leo imeachana rasmi na wachezaji wake Pape N’daw raia wa Senegal na Saimon Sserunkuma raia wa Uganda ndani ya klabu hiyo baada ya kujiridhisha na mwenendo mbovu wa wachezaji hao.


Akizungumzia kuachwa kwa wachezaji hao Afisa habari wa msimbazi Simba HAJI MANARA amesema uongozi umeridhia na kuamua kuachana na wachezaji hao baada ya kupokea ripoti ya kocha Mkuu wa klabu hiyo DYRAN KERR kutowahitaji ndani ya kikosi chake kwa hivi sasa.


MANARA amesema pamoja na kuachana na wachezaji hao klabu yao inamipango ya kuongeza wachezaji wengine ndani ya klabu hiyo katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili hasa kumuongeza aliyekuwa mchezaji wao PAUL KIONGERA na wachezaji wengine.

Kwa upande mwingine MANARA amefunguka kuhusu mipango na maendeleo ya uwanja wao uliopo maeneo ya Bunju huku akiwapuuzi wale wanaoibeza klabu hiyo kuhusu maendeleo ya uwanja wa klabu hiyo kushindwa kuujenga kwaajili ya matumizi ya wachezaji wake.

Aidha klabu ya soka ya simba inaendelea na mazoezi yake kwaajili ya mzunguko mwingine wa ligi kuu soka Tanzania bara.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget