Klabu ya Leicester City na Manchester City zimemaliza
mechi zao za Ligi Kuu soka nchini Uingereza kwa kupata matokeo ya bila
kufungani zilipokutana usiku wa kuamkia hii leo.
Leicester baada ya kucheza mchezo wake wa jana sasa
imefikisha pointi 39 sawa na Arsenal, lakini inabaki katika nafasi ya pili kutokana
na tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Klabu ya Man City wao wanakuwa katika nafasi ya tatu
palepale safari hii wakiwa na pointi 36 katika msimamo wa ligi hiyo.
Post a Comment