
Shirikisho la Mpira nchini Tanzania TFF imeiiomba
Serikali kwa kupitia Wizara ya habari,wasanii,utamauni na Michezo kushirikiana
kwa karibu katika kuandaa timu za Taifa na kuboresha miundo mbinu ya michezo
nchini ili kupata wachezaji wengi wenye vipaji wanotokea nchini kuanzia ngazi
ya chini.
Rais wa TFF Jamal Malinzi amesema kama wakipewa
fursa na Serikali kuratibu na kusimamia mpira wa miguu katika mashindano ya
Taifa ya shule za msingi (UMITASHUMTA) na Sekondari (UMISETA) wanaamini
wataongeza uweledi katika usimamizi huo na kuhakikisha vipaji vinaibuliwa kila
mwaka kuliko ilivyo hivi sasa.
Katika hatua nyingine Malinzi ameelezea mipango na
mikakati yao ya mwaka ujao katika kuboresha mchezo wa soka na kuufanya uwe
mchezo ambao unaleta maendeleo kuanzia ngazi ya chini ya vijana ambako kuna
vipaji vingi.
Post a Comment