
Serikali imetoa Baraka zake kwa mshambuliaji nyota
wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars, Mbwan Samatta baada ya kupata ulaji
wa kusajiliwa na klabu ya soka ya Genk ya nchini Ubelgiji.
Samatta mapema leo hii alitembelea Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo huku akiwa na mwenyeji wake Nape Nnauye na kupewa
bara hizo za kunda ulaya kucheza soka lake.
kwa upande wake Waziri Nnauye amesemaSerikali
itamuunga mkono mchezaji huyo baada ya konyesha umahiri wake katika kandanda na
kuitangaza nchi ya Tanzania kiamataifa.
Samatta ameishakubaliana na klabu ya Genk ya
Ubeligiji na sasa limebaki suala la Genk kumalizana na TP Mazembe ili January
mwakani aweze kuhamia moja kwa moja klabuni hapo.
Post a Comment