Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

ARSENAL KUPEWA VIBONDE SUNDERLAND KATIKA MICHUANO YA KOMBE LA FA MZUNGUKO WA 3.



 
Mechi za Mzunguko wa 3 wa Kombe la FA, ambalo kwa sasa linaitwa Emirates FA Cup ambalo huzikutanisha Klabu za Ligi Kuu England na Daraja la kwanza Mechi zake zitachezwa mwishoni mwa wiki hii.


Mabingwa Watetezi wa michuano hiyo klabuu ya Arsenal baada ya kulitwaa Kombe hili kwa mara ya pili mfululizo Jumamosi watakuwa katika uwanja wao wa nyumbani wa Emirates kuwakaribisha Sunderland.

Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu soka nchini England, Chelsea, Jumapili watakuwa kwao Stamford Bridge kucheza na timu ya Daraja la chini Scunthorpe United.

Jumamosi mashetani wekundu klabu ya Manchester United watakuwa nyumbani katika uwanja wao wa Old Trafford kucheza na Sheffield United, na Man City watakuwa ugenini kucheza na Norwich City.

Liverpool wao watafungua dimba Ijumaa wakiwa Ugenini kuivaa Exeter City huku Jumapili Tottenham wakiwavaa Leicester City ambao wako nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi kuu ya England.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget