Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SAFARI YA MBWANA SAMATTA YAIVA,KESHO HUYOO... KUELEKEA NIGERIA.



http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/05/cover2.jpg 
Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars na klabu ya soka ya TP Mazembe ya DRC Congo Mbwana Samatta kesho anasafiri kuelekea nchini Nigeria kushiriki katika sherehe za ugawaji tuzo za mwana soka bora wa Afrika zilizoandaliwa na chama cha soka barani Afrika CAF.


Samatta anasafiri kesho alfajiri kuelekea Nigeria akiongozana na katibu Mkuu wa Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF Mwesigwe Selestini  katika mji wa Abuja ambapo sherehe za utoaji tuzo hizo zitafayika  Alhamisi Januari 7, ambapo siku ya sherehe hizo Katibu Mkuu ataambatana na Ofisa ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria.

Afisa habari wa TFF Baraka Kizuguto amesema Mbwana Samatta anawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, huku pia akiwa mfungaji bora wa michuano ya Ligi ya Mabingwa (CAF CL) baada ya kuifungia klabu yake ya TP Mazembe mabao 8 na kuibuka mabingwa wapya wa michuano hiyo.

Samatta anawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika pamoja na mlinda mlango wa TP Mazembe, Robert Kidiaba (Congo DR) na mshambuliaji wa Etoile du Sahel Baghdad Boundjah (Algeria).

 

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget