Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

LEO NYASI LAZIMA ZIWAKE MOTO UKIZIKUTANISHA TIMU HIZI.



 

Klabu ya soka ya Yanga na Azam leo zitashuka kwenye dimba la Uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar kucheza mechi ya michuano ya Kombe la Mapinduzi, Mechi hiyo inatarajiwa kuwa ya vuta nikuvite kutokana na ushindani wa timu zenyewe.


Kila timu inataka kuonesha ubabe kwa mwenzie baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 katika mechi ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu bara mwaka jana

Klabu ya Azam inaongoza katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 35 huku klabu ya Yanga ikishika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 32.

Mechi ya leo pia inasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka hasa kutokana na matokeo yaliyopita ya mechi hizo ambapo Yanga iliifunga Mafunzo mabao 3-0 huku Azam ilipata matokeo ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Mtibwa.

Mechi nyingine itakayopigwa siku  ya leo itakuwa kati ya Mtibwa na Mafunzo.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget