
Aliyekua Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Simiyu, Epaphra Swai anatarajiwa kuzikwa leo jioni saa 10 katika kijiji cha Sawe, Masama Mashariki.
Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu itafanyika leo Jumamosi saa 9 alasiri, kitongoji cha Ituuny kijiji cha Sawe, na mazishi yake yatafanyika katika eneo la KNCU kata ya Masama Mashariki.
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) linaendelea kutoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki, wadau wa mpira wa miguu pamoja na familia ya marehemu, katika kipindi hiki kigumu cha maombelezo ya msiba huo.
Marehemu Epaphra Swai aliaga dunia Alhamisi asubuhi katika hospital ya taifa ya Muhimbili.
Post a Comment